Tuesday, April 10, 2012

KANUMBA ALIVYOAGWA KATIKA VIWANJA VYA LEADERS LEO:



Jeneza lenye Mwili wa Marehemu,Steven Kanumba likiwasili kwenye Viwanja vya Leaders Club,jijini Dar es Salaam asubuhi hii.
Makamu wa Rais,Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Steven Kanumba asubuhi hii kwenye viwanja vya Leaders Club,Jijini Dar es Salaam.akifuatiwa na Mkewe,Pamoja na Mke wa Rais,Mama Salma Kikwete (mwenye nguo nyeupe kulia).
 Mke wa Rais,Mama Salma Kikwete akiwasili viwanjani hapa. 
Mwili wa Marehemu Kanumba ukiwa mbele ya maelfu ya watu kwa ajili ya kuagwa rasmi
 
 Mbunge wa mbeya Mjini(CHADEMA)Joseph Mbilinyi aka Mr II Sugu akitoa heshima zake za mwisho.
Mwili wa Marehemu Steven Kanumba ukiwa umekwishawasili kwenye viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar mapema hii asubuhi tayari kwa watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali kuanza kuuaga mwili.
 
 
 Watu mbalimabli wakiwa wamezimia.Picha na Habari na Mdau Jestina George, Jeff Msangi.

No comments:

Post a Comment