Saturday, March 24, 2012

SERIKALI YA CHINA YAIPA MKOPO NAFUU SERIKALI YA TANZANIA, TSH.BILIONI 80:

Naibu Waziri wa Biashara wa China Li Jinzao (aliyesimama ) akitoa hotuba jana jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kusaini mkopo na misaada kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa ajili ya kuisaidia Tanzania. Sherehe hizo zilisainiwa na Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo (hayupo pichani)kwa niaba ya Tanzania na Naibu Waziri wa Biashara wa China Li Jinzao. Kulia ni Balozi wa China nchini Lu Youqing.
 Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo(aliyesimama ) akitoa hotuba jana jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kusaini mkopo na misaada kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China. Sherehe hizo zilisainiwa na Waziri Mkulo kwa niaba ya Tanzania na Naibu Waziri wa Biashara wa China Li Jinzao (hayupo pichani) . Msaada na Mkopo huo unazidi bilioni 80 Fedha za Kitanzania. Kushoto ni Waziri wa Uchukuzi Omar Nundu na kulia ni Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja.
 Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo(kushoto) na Naibu Waziri wa Biashara wa China Li Jinzao (kulia) wakisaini makubaliano leo jijini Dar es salaam ya Serikali ya China kuipa mkopo nafuu na msaada kwa ajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo nchini. Msaada na mikopo hiyo ni zaidi bilioni 80 fedha za Kitanzania ambayo inazidi kuimarisha urafiki na undugu kati ya Tanzania na China.
Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo(kushoto) akibadilishana mawazo na Naibu Waziri wa Biashara wa China Li Jinzao (kulia) leo jijini Dar es salaam wakati kiongozi huyo alipokwenda Wizara ya Fedha kwa ajili ya kusaini mkataba wa mkopo nafuu na msaada wa zaidi ya bilioni 80 za Kitanzania kwa ajili ya kusaidia shughuli mbalimbali za maendeleo nchini.

No comments:

Post a Comment