Sunday, February 5, 2012

UNGEPENDA KUSAIDIA; MAWAZO YAKO NI MUHIMU:

Nna tatizo naomba msaada kwa wana blog pls.
Mimi ni single mum nna mtoto wa kike miaka mitatu, nafanya kazi kijijini na NAHITAJI MWANANGU APATE ELIMU BORA.
Napanga kumpeleka mwanangu huyu shule ya bweni kwa umri alionao naumia roho ila kwa mazingira nnayoishi nimeonelea nimpeleke tuu, but b4 doing tht naomba pia nipate maoni ya wadau humu kama kuna experience tofauti au kuna vitu nahitaji kuangalia kabla ya kufanya maamuzi hayo.
Natamani sana nikae nae mtoto huyu, ila kuna changamoto kadhaa zinanikumba, kwanza, im single na babaake hana msaada kabisa na mtoto, pili, natoka home alfajiri sana na kurudi usiku, tatu, wasichana wa kazi hawatulii maana huku kuna midume kibao akifika tuu mara katoroshwa!!
Nmeshabadili wasichana wa kazi kama wanne ndani ya mwaka jana tuu!!! so inaniwia vigumu kuamua, je niendelee kumbadilishia wasichana au nimpeleke shule akiwa mdogo tuu hivi!!
Mnaweza nambia nimpeleke kwa ndugu, sawa. Lakini hali halisi ya familia na ndugu zangu ni ya ajabu naweza sema, hakuna mtu yuko tayari kulea mtoto wa mwenzie!! hata mm im not ok kumwacha kwa ndugu maana nahisi nikikuta yuko tofauti na matarajio undugu waweza kuisha!!!
Im confused jaman, naombeni tuu msinitukane na mnipe ushauri maana nipo njia panda.
ASANTENI.
---------------- Ndugu, Mawazo yako ni muhimu-------------------
NB: Kwa mwenye shida binafsi na ungependa ionekane, wasiliana nasi kwa kutuma email kwenda; carishapa@gmail.com

1 comment:

  1. Mwanao ana umri gani? Labda tuanzie hapo kabla ya hatua inayofuata ya ushauri..

    ReplyDelete