Tuesday, January 31, 2012

HATIMAYE MWANZA KWANZA WAFIKISHA RAMBI RAMBI ZAO KWA MAMA WA MAREHEMU MSANII MO-CHELA ALIYEUAWA MWEZI ULIOPITA:



Kutoka kushoto ni Wasanii wa Rock City 'Mwanza Kwanza' J.Aden, Rajabu, G.Rico, Sisar Madini, Sajna, PMP Silva, Festudo na Shira wakiwa safarini na meli ya Mv Nyehunge kuelekea Ukerewe Nyumbani kwao marehemu Mo-Chela ambako ndiko alikozikwa nia ikiwa ni kuwasilisha rambirambi zao kwa mama wa marehemu.Wawakilishi hao walifika salama salmini kisiwani Ukerewe.Safari kuelekea makaburi ya ukoo wa marehemu.Hapa ndipo ulipolala mwili wa Mo-Chela.Mara baada ya kukamilisha ratiba ya sala 'Wanamwanza Kwanza' walikusanyika nyumbani kwao marehemuMtangazaji wa Kiss Fm Ezden The Rocca akiwa na Janet Buchela ambaye ni dada wa marehemu kwenye familia yao walizaliwa wawili tu hivyo dada huyu kaachwa mpweke. Mwenyekiti wa Mwanza Kwanza Philbert Kabago akimkabidhi rambirambi Bi. Prudenciana Ngereza ambaye ni mama mzazi wa marehemu Mo-Chela kiasi cha shilingi 500,000/= fedha taslimu ambapo kabla fedha nyingine zilitumika katika ujenzi wa kaburi shilingi 152,000/=, kundi lake alilokuwa akiimbia lilichangiwa shilingi 100,000/= na huduma nyingine muhimu za kukamilisha msiba.Chakula cha pamoja kiliandaliwa na mama yetu nayo menyu ilikuwa ni full kujisevia. "Usiseme kAMA nInaPeNDa kULa..!!" @Sajna Mkali wa rnb Bongo Fleva aliyeshiriki vyema kuhakikisha zoezi zima linafanikiwa .
Marehemu Mo-Chela alipokuwa kuwa mdogo miaka miwili hivi....Marehemu alipokuwa mchanga....Marehemu Mo-Chela katika majukwaa yake ya mwanzoni hapa ilikuwa Laverna Beach 2009.Marehemu katika swagga alikuwa wamo......Enzi za uhai wake Marehemu Mo-chela katika picha ya pamoja na mama yake mzazi.Sissar Madini akisaini autografu' za masupastaa wa kesho wa pande za UK'

No comments:

Post a Comment