Friday, August 12, 2011

MWANDUSHI WA HABARI, RICHARD MASATU, AUWAWA KIKATILI:


MAREHEMU RICHARD MASATU.
Imenichukua muda kuamini (zaidi ya saa 24), pengine hii ndiyo sababu ya kuchelewa kuwafahamisha kuwa Tasnia ya Habari Mwanza imepata pigo kubwa baada ya Mwandishi wake mahiri Richard Masatu ambaye pia alikuwa Mkurugenzi wa Gazeti la KASI MPYA kufariki Dunia akiwa anapatiwa Matibabu katika Hospitali ya Mkoa ya Sekou Toure.

Taarifa za awali zinaonyesha kuwa Marehemu amekufa kutokana na majeraha ya kushambuliwa na watu wasiojulikana. Kwa sasa mwili wake upo Hospitali ya Rufaa ya Bugando mara baada ya uchinguzi uliofanyika jana kwa zaidi ya saa kadhaa kutokana na kukutwa na majeraha ya kuchomwa na kitu chenye ncha kali, chini ya Kidevu, jicho la kulia ikiwa na kupigwa na kitu kizito usoni upande wa kushoto.

Baada ya kukamilika kwa uchunguzi, mwili wa marehemu utaagawa kesho Ijumaa saa 3 asubuhi nyumbani kwake Nyakato na kisha kusafirishwa kwenda Bunda mkoani Mara kwa mazishi.
EWE MWENYEZI MUNGU MSIMAMIE MJA WAKO
AMEN.

No comments:

Post a Comment