Monday, May 30, 2011

MERCYJOY NYAGWASWA AZINDUA CD NA DVD ALBAM YA NYIMBO ZA INJILI:


Hapo juu ni kikundi cha nyimbo za injili cha "RC Choir" cha jijini Mwanza wakiwa stejini wakimsindikiza Bi.Mercyjoy Paul Nyagwaswa katika tamasha la uzinduzi wa albam yake (CD na DVD) ya nyimbo za injili aliyoipa jina la "LANGO".

Uzinduzi huo ulifanyika jana tarehe 29 May 2011 katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ambapo, mbali na mgeni rasmi sambamba na wageni wengine waalikwa, uzinduzi huo ulipata pia baraka nyingi kutoka vikundi mbalimbali vya nyimbo za injili vya jijini Mwanza ambavyo vilijitokeza jukwaani kusindikiza uzinduzi huo.

  RC Choir wakionesha cheche zao jukwaani.


 Mwanza Choir nao walikuwepo.


 Upande wa 'Microphone' wa Mwanza Choir.

 Nuru Choir - Butimba.


 Upande wa 'Microphone' wa Nuru Choir.

 Muungano Choir - Igoma.

 Muungano Choir wakichanja mbuga.





 Wanafunzi kutoka kikundi cha watoto yatima nao walikuwepo katika usindikizaji.

 Wanafunzi wakifanya mambo yao.

 Picha ya wanafunzi iliyopigwa kwa juu.

 Upande wa 'jikoni' huku tunamwona kaka hapo akilicharaza Gitaa.

Mr.Promo, MC wa shughuli hiyo, mzuka ulimpanda nae ikabidi apande jukwaani kufanya vitu vyake. Aaah aaah, so soooo funny. Ilipendeza sana.


Jukwaani watu walijaa kama inavyoonekana.

Meza kuu, mgeni rasmi (Wapili toka kushoto), mkuu wa wilaya ya Sengerema anayefuata kulia kwa mgeni rasmi ni baba mzazi wa Mercy, Askofu mkuu mstaafu wa African Inland Church (AIC) Tanzania - Dr. Metusellah Paul Nyagwaswa. Wengine ni wageni waalikwa wa shughuli hiyo.

 Wachezaji wa Mercyjoy Nyagwaswa wakiingia jukwaani kwa staili ya 'Break Drance' tayari kwa kuanza mambo ya uzinduzi wenyewe.

 Bi. Mercyjoy Paul Nyagwaswa (Katikati mbele) akiongoza 'jeshi' lake jukwaani.

 Hapa wakiimba wimbo unaoitwa 'POPO'.

 Popo, popo popo, the song was so melodious.

 Mercy akisoma risala.

Wakikumbushia kipande cha wimbo fulani uliopatwa kutajwa katika risala hiyo uliowahi kutungwa na Mercy siku za nyuma mahsusi kabisa kwa maombolezo ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwl J.K Nyerere, siku chache baada ya kifo chake.

Zawadi kwa baba. Mercy akimwagiza moja kati ya vijana wake apeleke zawadi kwa baba yake mzazi aliyekaa kwenye meza ya wageni waalikwa.
Baba huyo akipokea zawadi kutoka kwa mtoto.

Mercy akimkabidhi mgeni rasmi copy ya risala iliyosomwa.

Kumbe ile ilikuwa ni trela tu sasa picha kamili ndiyo hii, kwa mikono yake, Mercy akimkabidhi baba zawadi aliyomwandalia kama shukrani kwa yote aliyomtekelezea mpaka kufikia hapo alipo, hatua ya kuzindua albam yake ya kwanza.

Akisalimiana na mtoto.
Miongoni mwa waimbaji wazuri wa nyimbo za injili wa sasa, all the way from Dar es salaam to Mwanza, Martha Mwaipaja, naye alikuwepo kutoa support yake katika uzinduzi huo. Safi sana, urafiki uliotukuka huu.

Martha keeps on rocking the crowd.

Meza kuu sasa imehamia chini kwa ajili ya uzinduzi kamili.
Baba, askofu mkuu mstaafu wa AIC, Dr Metusellah Paul Nyagwaswa akiongea machache na hatimaye kumkaribisha mgeni rasmi Mh. Mkuu wa wilaya ya Sengerema ili aendelee na shughuli nzima.


Mheshimiwa akiongea yake machache.
Mercy akimkaribisha mgeni rasmi akate utepe kama ishara ya uzinduzi wa albamu hiyo.

Mgeni rasmi akikata utepe.
Utepe umeshakatwa sasa tugawane vilivyomo, Mercy akimkabidhi mhemishimiwa mgeni rasmi copy mbili za albam hiyo.
Akimshukuru kwa kuweza kuitikia mwito na kufanikisha zoezi zima la uzinduzi.
Mheshimiwa mgeni rasmi naye akishukuru kwa nafasi aliyopewa.
Kwanza tuombe, maombi hayo kutoka kwa baba.
Maombi yakiendelea.

Hapa Mr. promo akitangaza kiasi cha pesa cha Tsh.1,000,000/= kilichotolewa na baba akimuunga mkono mwanawe kwa kununua albam hiyo.

Mzee wetu nae akitangaza kiasi chake.


Mr.Promo akichungulia kiasi kilichotajwa na mzee wetu, kilikuwa ni Tsh.100,000/=.
Mama wa kizungu nae akitangaza kiasi chake.
Mama huyo nae hakubaki nyuma, kama kawaida.

Askofu wetu nae akitoa chake.

Mama huyo nae akito chochote chake.
Once again, back to the stage. Mercy akiimba wimbo uliobeba jina la albam, "LANGO".

"Lango" ukiendelea kutuburudisha.
Sasa ni ruksa kwa kila aliyekuwepo ndani ya ukumbi kucheza na kuimba kwa pamoja. Mercy na Martha walishirikiana kuimba wimbo huo na watu wote walinyanyuka pale walikokuwa wameketi wakajaa jukwaani kwa shangwe na nderemo. Makaka hao wakicheza sijui ni kuduku au ni nini, I don't know, ila ilinoga sana. Hatimaye albam ya dada Mercyjoy Paul Nyagwaswa inayitwa "LANGO" ikawa IMEZINDULIWA RASMI.

HISTORIA FUPI YA MERCYJOY NYAGWASWA:
EDUCATION BACKGROUND:
1981-1982: Oysterbay Primary School (Dar es salaam-Tanzania)
1983-1987: Nyakahoja Primary School (Mwanza-Tanzania)
1988-1989: Weruweru Girls High School (Moshi-Tanzania)
1989-1991: Moi Girls High School (Nairobi-Kenya)
1993-1998: University Of Eastern Africa (Nairobi-Kenya)
                    *Bachelor of Arts in Languages.


AWARDS:
Weruweru Girls High School: Solo of the year (2 times),
Moi Girls High School: Best Singer Trophy,
University Of Eastern Africa:  -The Most Active Person in all university activities,
                                             -The Most Active Person in all church activities.

WORK EXPERIENCE:
1999:           Coastal Television Network (CTN)
                    * English News
                    *News Editor

2000-2001: Vodacom Tanzania Limited
                    *Customer Care Personnel

2001-2004: Tanzania Broadcasting Corporation (TBC)
                    *English News

2001-2004: Clouds Fm Radio
                    *English News (Part time)

2007-2009: East Africa Radio and East Africa TV
                    *English News

2009-2011: The "LANGO" CD and DVD album Preparations.

The album "Lango" was cooked up to carry the following best mixed gospel hits:
1.  Lango  : Done at Soundcrafters studio, produced by Bizzman,
2.  Popo   : (Makeba style), Done at Amina studio, 
3.  Mpumbavu: (Kwaito style), Done at CVC studio, produced by Fabris,
4.  Utajiri  : (Reggae style),
5.  Kimbilio: (Traditional style), Done at Bigtime Studio, by Saidi Comorien,
6.  Utateseka: (Madiba style), CVC studio, produced by Fabris,
7.  Maadui : (Slow RnB style), CVC studio, produced by Fabris,
8.  Tumaini : CVC studio, Produced by Fabris,
9.  Yatima na wajane: CVC studio, produced by Fabris,
10. Mama : FM studio, Produced by Miika Mwamba,
11. Hakuna kama yesu: (Sebene style), CVC studio, produced by Fabris.
Note: To post a comment:
Click 'comment',write your comment in the comment pad,THEN (Select Anonymous profile to hide your name OR Name/URL profile to disclose your name ie Name: (Write your name) and URL: (This is optional)) THEN Click 'Post comment',type the word shown for verification THEN Click 'Post comment'.

4 comments:

  1. kumbe hata huko kwenu mwanza kuna mambo mazuri ya kumcha Mungu thru gospel ok mpo juu sana mkoa wangu.

    ReplyDelete
  2. stay blessed!! the work is so tough but through to worship god all things gonna be okay my mum!!!

    ReplyDelete
  3. i enjoy ur work of gospel!!! but we mic in media..! when gonna u be back...?

    ReplyDelete
  4. The Vintage Wholesale Company The Vintage Wholesale Company.Walson Rockabilly are a vintage wholesale company who focus on vintage fashion wholesale. WalsonRockabilly Vintage Clothing wholesalers are the UK's leading,Shop wholesale vintage dress, cheap silk dress, vintage jewelry products from reliable vintage dress wholesalers on walsonrockabilly and get worldwide,We know wholesale vintage clothing. We're the only vintage clothing wholesaler that knows what it's like to be in your shoes,because we run stores ourselves.Always Vintage is a Wholesale Vintage Clothing Distributor. We offer more than ninety different categories of vintage clothing for you to choose from.adult penguin costume
    mario luigi costume
    20s charleston flapper costume

    ReplyDelete