Thursday, May 19, 2011

DUUUH...!! HII NI FUNGA FUNGUA MWAKA:

Kama ni lumbesa sasa hii ni luuumbeeesaaa. Hii ni moja ya mifano ya wazi inayothibitisha kwamba Bongo mambo bado si shwari, kila kukicha bora ya jana. Nadhani 'mjomba' Mpoto hajapata ile nauli ya kumfikisha kwa mjomba wake na hatimaye kumdadafulia yanayotusibu sisi raia wa kawaida tunaoishi kwa kipato cha chini ya dola moja kwa siku, tunaokula mlo mmoja kwa siku, tunaokula tunachokipata na si tunachokitaka. Je, nani alaumiwe, ni serikali kwa kushindwa kutambua na kujali shida za wananchi wake au ni mwananchi kwa kuvunja kipengele cha sheria kinachopinga kutembeza gari chakavu barabarani, mbaya zaidi likiwa limebeba mzigo uliozidi kiwango a.k.a Lumbesa?

Note: To post a comment:
Click 'comment',write your comment in the comment pad,THEN (Select Anonymous profile to hide your name OR Name/URL profile to disclose your name ie Name: (Write your name) and URL: (This is optional)) THEN Click 'Post comment',type the word shown for verification THEN Click 'Post comment'.

No comments:

Post a Comment