Chini ya ulinzi: Kulia ni mfanyakazi wa meli hiyo.
Mchezo huo mchafu ulistukiwa na mfanyabiashara maarufu jijini Mwanza bwana Kitana, ambaye pia ana miliki vyombo vya usafirishaji na uvuvi ziwani Victoria, mara baada ya kuona mazingira yasiyoeleweka alito taarifa kwa wamiliki wa meli ya Mv. Allez ambao kwa haraka walipanga mchakato wa mtego na siku iliyofuata walifanikiwa kushuhudia wizi huo mwanzo mwisho live bila chenga jinsi unavyochezwa.
Watuhumiwa hao katika mahojiano wamesema kuwa wamekuwa wakijihusisha na mchezo huo kwa kipindi kirefu wakishirikiana na wafanyakazi wa meli hiyo nao hufanya zoezi hilo nyakati za usiku pindi meli zinapotoka safari, kwa kufyonza mafuta yaliyosalia mara baada ya meli kutoka safarini na hili hufanyika kabla meli haijaandikiwa mafuta kwa safari inayofuata.
Mpira wa kufyonzea ukiwa kwenye chanzo (matanki ya mafuta) melini.
Watuhumiwa wakiwa sambamba na mtuhumiwa namba moja mfanyakazi wa meli hiyo (wa tatu kutoka kushoto)
No comments:
Post a Comment