Monday, February 13, 2012

WASANII WARUDI KIJIJINI CHA MWANZEGA KIMBIJI TARAFA YA MKURANGA CHINGUNGWENI MKOA WA PWANI:


Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) Cassim Taalib (katikati) akimwelekeza Sheikh Majaliwa Selemani aliekwenda kuangalia maendeleo ya kijiji cha Mwanzega Mkulanga Tarafa ya Chingungweni, zinapojengwa nyuma kwa ajili ya wasanii Sheikh Majaliwa , alitoa Ahadi ya kujenga Msikiti na Madrasa itakayofadhiliwa na African Relief Comettee Kuwait.
Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) Cassim Taalib (kulia) akiwa na wajumbe pamoja na viongozi wa mtandao huo walipokwenda kuangalia ujenzi unaoendelea wa nyumba zao, katika kijiji cha Mwanzega Kimbiji Tarafa ya Mkuranga Chingungweni Mkoa wa Pwani jana wa pili kulia ni Ahmed Olotu 'Chilo' Kikumbi Mwanza Mpango ' King Kiki' Katibu wa mtandao huo, Selemani Pembe.
Waandishi wa habari za michezo pamoja na wasanii, wakitembea kwa ajili ya kwenda kuangalia ujenzi unaoendelea wa nyumba zao, katika kijiji cha Mwanzega Kimbiji Tarafa ya Mkuranga Chingungweni Mkoa wa Pwani jana kutoka kulia ni Tomm Chilala, Kibwana Dachi na Kikumbi Mwanza Mpango ' King Kiki'.

No comments:

Post a Comment